Na Editha Karlo- Globu ya Jamii Kigoma

RAIS Wa Jamuhuri wa Muungano Wa Tanzania Dkt John Magufuli amempongeza aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini ,David Kafulila kwa kujitoa Muhanga kutetea Watanzania kupitia sakata la Escrow(IPTL) na kuonesha uzalendo Mkubwa ambao hawezi kusahaulika katika historia ya Tanzania.

Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Nguruka,leo Katika uzinduzi wa Mradi mkubwa wa Maji uliopo Tarafa ya Nguruka katika Wilayani Uvinza, alisema atakuwa mnafiki akishindwa kumpongeza Kafulila kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuibua Ubadhilifu uliofanywa na Kampuni ya IPTL ambapo kwasasa suala hilo ameanza kulifanyia kazi na mafanikio yameanza kuonekana.

Amesema Kafulila alitukanwa sana alipo ibua sakata la Escrow na kuitwa majina mengi ya kudhalilishwa kama tumbili na mengine mengi ya ajabu kwasababu ya uzalendo wake wa kutetea Taifa.

"Mimi ninafahamu unapoibua kitu cha kizalendo lazima usemwe, hivyo ninampongeza Kafulila kwa uzalendo wake kwa nchi na nitaendelea kumpongeza maisha yangu yote"alisema Magufuli.Magufuli alisema maendeleo hayana chama ndio maana Kafulila alijitoa kwa hali ya juu na kutetea fedha za Wananchi zilizo kuwa zikiibiwa na mafisadi wachache na kujinufaisha wao.

"Ninajua Kafulila ulitukanwa sana wakati wa kuibua sakata la Escrow, wapo watu walikuita tumbili mimi najua wewe sio tumbili ,matumbili ni wao wewe najua ni wa Chama kingine lakini umefanya kazi kubwa ya kulinda maslahi ya nchi, kwahiyo nitakuwa mnafiki sana nisipo kupongeza kitu ulichokifanya ni kikubwa Kwa,Taifa naomba nikupongeze kwa hilo",

Alisema Kiongozi mzuri ni yule ambae anatetea wananchi bila kujali chama wala siasa za uchochezi , hivyo atahakikisha kuwa Wananchi hawateseki na Wale ambao wameiba fedha za serikali na Wananchi wanazirudisha bila kujali nyadhifa walizonazo, ili pesa hizo zitumike katika kuleta maendeleo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Mh.David Kafulila

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...