Mbunge wa mkuranga ,Abdallah Ulega akizindua madarasa yaliyojengwa kwa ushirikiano na familia ya Ghulam Hussein pamoja na mdau wa maendeleo na balozi wa heshima kutoka visiwa vya Seychelles Maria Van Pool (aliyevaa nguo nyekundu).

 Mbunge wa Mkuranga  Abdallah Ulega amefanikiwa kuzindua madarasa mawili katika shule ya msingi Muongozo kijiji cha Mwarusembe yaliyojengwa kwa hisani ya familia ya Ghulam Hussein ikiwa ni kuitikia ombi la Mbunge la kushirikiana na wadau mbalimbali katika  kuijenga Mkuranga.

Familia hii imeunganishwa na mdau wa maendeleo na balozi wa heshima kutoka visiwa vya Seychelles Maria Van Pool na Katika uzinduzi huo  Ulega aliwasisitiza wazazi kusimamia vyema maendeleo ya elimu ya watoto kwa kushirikiana na walimu.

Mbunge Ulega alisisitiza pia kutunzwa kwa miundombinu ya elimu ili iweze kudumu kwa mda mrefu na kuwanufaisha waTanzania walio wengi                       

  Mbunge wa jimbo la Mkuranga,Abdallah Ulega akizungumza na wazazi pamoja na wanafunzi katika hafla ya uzinduzi wa madarasa mawili katika shule ya msingi Muongozo kijiji cha Mwarusembe, Madarasa hayo yamejengwa kwa hisani ya familia ya Ghulam Hussein.                        

Muonekano wa nje wa madarasa hayo, pamoja na Mbunge wa mkuranga ,Abdallah Ulega akiwa pamoja na  familia ya Ghulam Hussein pamoja na mdau wa maendeleo na balozi wa heshima kutoka visiwa vya Seychelles Maria Van Pool na wanafunzi wa shule wakiwa wamekaa katika madawati ndani ya madarasa hayo.
 Mbunge wa mkuranga ,Abdallah Ulega akisalimiana na wazazi na  wanafunzi  katika hafla ya uzinduzi wa madara mawili katika shule ya msingi Muongozo kijiji cha Mwarusembe, Madarasa hayo yamejengwa kwa hisani ya familia ya Ghulam Hussein

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...