Hyasinta Kissima-Njombe.

Shirika la kulinda na kutetea haki za watoto dunia UNICEF limetoa vifaa vya aina mbalimbali vyenye thamani ya Shilingi Milioni 4,591,000/= kwa makundi matatu ya watoto wenye mahitaji maalumu katika Halmashauri ya Mji Njombe.

 Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda amesema kuwa anaipongeza UNICEF kwani wamekuwa wadau wakubwa wa maendeleo katika halmashauri yake sio kwa upande wa lishe kwa watoto bali hata kujali makundi ya watoto wenye mahitaji maalumu.

Aidha Mkurugenzi huyo amevipongeza vyombo vya habari kwa kuandika habari mbalimbali za kijamii kwani kupitia habari za shughuli za kijamii zilizokuwa zinaandikwa na vyombo vya habari shirika la UNICEF liliguswa na kuona ni vyema kuunga mkono jitihada hizo.

“Ninaamini kabisa Kwa jitihada za waandishi wa habari kutangaza habari ambazo huwa tunatoa misaada kidogo kidogo ile ya Halmashauri kila robo ya mwaka kwa vituo mbalimbali vya kulelea watoto habari ziliwafikia wenzetu wa UNICEF nao wakaona ni vizuri wakatuunga mkono”Alisema Mwenda.
 Mkurugenzi wa Halmasahuri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda (wa kwanza kushoto) akisoma taarifa ya vifaa vilivyokabiidhiwa kutoka UNICEF
 Sehemu ya watoto  wenye mahitaji maalumu kutoka shule ya Msingi Ramadhani, Kibena na Kituo cha Kulelea watoto Yatima cha Compassion waliofika kwenye makabidhiano hayo
 Msaada wa Vifaa kwa watoto wenye mahitaji maalumu kutoka UNICEF.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...