WADAU katika sekta ujenzi nchini wametakiwa kutumia bidhaa zenye viwango na ubora unaostahili ili kulinda ukuaji wa sekta hiyo na kuleta matokea chanya kwa ustawi na maendelea ya taifa na watu wake.

Akizungumza kwenye semina iliyowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wahandisi, makandarasi, wazalishaji, wasambazaji na watumiaji wa nyaya za umeme jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwango wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Bi. Edna Ndumbaro alisema bidhaa zinazotumika kwenye masuala ya umeme zinahitaji kuwa na viwango na ubora unaostahili.

“Badiliko la rangi mpya za nyaya za umeme (New Colour Codes) limewaleta wadau hawa muhimu kujadiliana kwa pamoja na kuazimia kwa pamoja namna bora ya utekelezaji wake,” Bi. Ndumbaro alisema. Alisema rangi mpya ya nyaya ya umeme ilishaazimiwa kama kiwango cha lazima kufuatwa tangu mwaka 2016 na hivyo ni vyema kwa wadau na wataalamu wakazingatia kuwa viwango ni jambo muhimu sana likapewa kipaumbele zaidi.

“Sisi kama TBS tutaendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa viwango na ubora kupitia vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii ikiwemo tovuti ya shirika,” Bi. Ndumbaro alisema na kuongeza kuwa washiriki wa semina hiyo watakuwa walimu wazuri.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwango wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Bi. Edna Ndumbaro akisisitiza jambo kwenye Semina ya wadau kwenye semina iliyowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wahandisi, makandarasi, wazalishaji, wasambazaji na watumiaji wa nyaya za umeme jijini Dar es Salaam jana kuhusu matumizi ya Rangi mpya za nyaya za umeme.
Afisa Viwango wa Viwango wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Bw. Henry Massawe akiwasilisha mad kwenye Semina ya wadau kwenye semina iliyowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wahandisi, makandarasi, wazalishaji, wasambazaji na watumiaji wa nyaya za umeme jijini Dar es Salaam jana kuhusu matumizi ya Rangi mpya za nyaya za umeme.

Baadhi ya washiriki wa semina ya wadau kwenye semina iliyowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wahandisi, makandarasi, wazalishaji, wasambazaji na watumiaji wa nyaya za umeme jijini Dar es Salaam jana kuhusu matumizi ya Rangi mpya za nyaya za umeme semina hiyo imeandaliwa na Shirika Viwango wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...