JESHI la Polisi  Mkoa wa Pwani  wamewakamata watuhumiwa wawili  ambao wameshikwa  wakisafirisha  dawa za kulevya  aina ya Bhangi  magunia nane.
 Watuhumiwa hao walionaswa  na Jeshi la Polisi wamefahamika  kwa  mjina Abraham Michael  mwenye umri wa miaka  31 mkaazi wa Jijini Dar es Salaam na Godfrey  Malakasuka  mwenye umri wa miaka 21 mkaazi wa Kimara  waliokamatwa katika eneo la Ubena Zomozi wakitokea Mkoani Morogoro kuelekea Jijini Dar es Salamaa.
Akizungumza na  waandishi wa habari  Kamanda wa Mkoa wa Pwani ACP Jonathan Shanna  alisema kuwa watuhumiwa  wamekamatwa na vidhibiti  hivyo wanastahili  kupata adhabu kali pindi watakapofikishwa  mahakamani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...