JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani wamewakamata watuhumiwa wawili ambao wameshikwa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Bhangi magunia nane.
Watuhumiwa hao walionaswa na Jeshi la Polisi wamefahamika kwa mjina Abraham Michael mwenye umri wa miaka 31 mkaazi wa Jijini Dar es Salaam na Godfrey Malakasuka mwenye umri wa miaka 21 mkaazi wa Kimara waliokamatwa katika eneo la Ubena Zomozi wakitokea Mkoani Morogoro kuelekea Jijini Dar es Salamaa.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Mkoa wa Pwani ACP Jonathan Shanna alisema kuwa watuhumiwa wamekamatwa na vidhibiti hivyo wanastahili kupata adhabu kali pindi watakapofikishwa mahakamani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...