WANANCHI wa wilaya ya Muheza mkoani Tanga wataondokana na adha ya huduma ya maji baada ya Serikali kutenga fedha zaidi ya milioni 400 kwa ajili mradi mkubwa wa kutoa maji kutoka eneo la Pongwe Jijini Tanga hadi wilayani Muheza.

Hatua hiyo ina lenga kuondoa changamoto ya uhaba wa maji wilayani Muheza ambayo ilikuwa kikwazo cha maendeleo kwa wananchi kutokana na kutumia muda mwingi kusaka huduma hiyo badala ya kufanya shughuli za kujiingizia kipato.

Akizungumza jwakati wa kukabidhi mabomba yatakayotumika kwa mkandarasi wa mradi huo katika eneo la Pongwe Jijini Tanga, Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu alisema mradi huo utakuwa ndio mkombozi mkubwa kwa wananchi.

Alisema mradi huo ambao ni mkubwa ni moja kati ya ahadi za Rais John Magufuli alipofanya ziara mkoani Tanga ambapo alihaidi kuhakikisha wakazi wa mji huo wanaondokana na changamoto ya uhaba wa maji.

"Kwanza nimshukuru mh Rais kwa kutekeleza ahadi yake mapema jambo ambalo limetupa faraja kubwa sisi wakazi wa Muheza na vitongoji vyake lakini niwaambie katika mradi huu nitakuwa mkali sana na nitafuatilia kila mwezi kuhakikisha unajengwa kwa viwango kutokana na thamani ya fedha"Alisema.
Mhandisi wa Mradi wa Maji kutoka eneo la Pongwe Jijini Tanga hadi wilayani Muheza kutoka kampuni ya Koberg Construction Co.Limited Mhandisi Stepheni Kingili kushoto akitoa maelekezo kwa Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu namna watakavyoanza kutekeleza mradi huo kuanzia kesho(leo) wakati wa halfa ya makabidhiano ya vifaa vya mradi huo yaliyofanyika ofisi ndogo za mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) eneo la Pongwe
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa akiingia kwenye halfa hiyo
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajaabu wa pili kutoka kulia akiongozana na baadhi ya viongozi kukagua mabomba yatakayotumikaa kwenye mradi huo kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Luiza Mlelwa na kushoto ni Mhandisi wa Mradi huo ambao utatoa maji Pongwe Jijini Tanga Hadi wilayani Muheza
Moja kati ya vifaa mbalimbali vitakayotumika kwenye mradi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...