Baada ya Kampuni ya uchimbaji wa Madini ya African Barrick Gold Mining, kuonyesha nia njema ya kuendelea kuwekeza nchini, Umoja wa vijana wa (CCM) mkoa wa Mwanza (UVCCM), umempongeza Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa jitihada za kusimamia rasilimali za Taifa.
Umoja huo umetoa tamko hilo baada ya Kampuni hiyo kuipatia Tanzania shilingi Billion 700, ikiwa ni njia ya kuthamini makubaliano yaliyohafikiwa kati ya Serikali na Kampuni hiyo, ambayo kwa sasa inajipanga kukamilisha deni lake la la zaidi ya shilingi Tririoni mia nne.
Viongozi wa Umoja wa vijana wa (CCM mkoa wa Mwanza (UVCCM), wakitoa tamko hilo la pongezi kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli, kwa jitihada za kusimamia rasilimali za Taifa ikiwemo madini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...