Helikopta iliyoanguka Ziwa Nakuru mara baada ya kuruka kutoka katika hoteli jirani na ziwa hilo Jumamosi hii asubuhi imepatikana lakini habari zinasema miili ya abiria watano waliokuwamo bado haijapatikana.

Habari zinazidi kueleza kwamba helikopta hiyo ilikuwa ikielekea kwenye mkutano wa kampeni wa chama cha Jubilee katika county ya Narok.
Ajali hiyo ilithibitishwa na kitengo cha Taifa cha maafa cha Kenya (NDMU). "Taarifa toka chanzo cha kuaminika ni kwamba kwa bahati mbaya helikopta binafsi imezama katika ziwa Nakuru, na inadhaniwa kwamba abiria na nahodha wake bado wangali wamenasa ndani yake.
"Juhudi za uokoaji zinaendelea na NDMU imeleta helikopta kusaidia zoezi hilo", Naibu Mkurugenzi wa NDMU Mwachi Pius amenukuliwa akisema.
Polisi bado haijatoa majina ya watu watano walikuwemo kwenye ajali hiyo hadi baada ya ndugu wao wa karibu kujulishwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...