Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeipiga kalenda kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili vigogo wa Kampuni ya mawasiliano ya Six Telecoms, akiwemo Wakili Dk Ringo Tenga na wenzake kwa sababu upelelezi bado haujakamilika.

Mbali na Dk. Tenga, washitakiwa wengine ni Mfanyabiashara Peter Noni, Mhandisi na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Hafidhi Shamte, Mkuu wa fedha wa kampuni hiyo, Noel Odeny Chacha na Kampuni ya Six Telecoms Limited.

Wakili wa Serikali, Leonard Challo alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi bado unaendelea.

Hakimu Nongwa aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 26, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.Katika kesi hiyo namba 73 ya 2017, inadaiwa kati ya January 1, 2014 na January 14,2016 Dar es Salaam washitakiwa, walitoza malipo ya simu za kimataifa kwa kiwango cha dola 0.25 kwa dakika kwa lengo la kujipatia faida.

Pia washtakiwa hao wanadaiwa katika tarehe hizo, washtakiwa waliisababishia TCRA hasara ya Dola za Marekani 3,736,861, sawa na Sh bilioni nane
Pichani ni Watuhumiwa wa kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili vigogo hao Watatu wa Kampuni ya mawasiliano ya Six Telecoms, akiwemo Wakili Dk Ringo Tenga na wenzake wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mapema leo .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...