Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza wakati akifungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watatu kulia), na Naibu Katibu Balozi Hassan Simba Yahya (wanne kulia), wakiimba wimbo wa mshikamano wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara .Wengine ni viongozi wa Chama cha Wafanyakazi tawi la wizara hiyo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Thobias Andengenye, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala na Kamishna wa Magereza anayeshughulikia Utawala na Fedha, Gaston Sanga wakiimba wimbo wa mshikamano wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara.Kikao hicho kimechofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala, akichangia hoja wakati wa
Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara
katika kutimiza majukumu ya wizara.Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi
wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo.Wengine ni
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Thobias
Andengenye(kushoto) na Kamishna wa Magereza anayeshughulikia Utawala na
Fedha, Gaston Sanga. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Thobias Andengenye,akichangia hoja wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara.Kikao hicho kimechofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo.Wengine ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala na Kamishna wa Magereza anayeshughulikia Utawala na Fedha, Gaston Sanga. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, akichangia hoja wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...