KAMANDA WA  WA MKOA WA MWANZA SACP LIBERTUS BARLOW (pichani) AMEUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NA WATU WANAOHISIWA KUWA NI MAJAMBAZI  KATIKA ENEO LA KITANGILI JIJINI HUMO  USIKU WA KUAMKIA LEO.

HABARI ZINASEMA MAREHEMU ALIUWAWA MAJIRA YA SAA TISA USIKU AKIWA NJIANI KUELKEA NYUMBANI KWAKE AKITOKEA KUMRUDISHA DADA YAKE  BAADA YA KUHUDHURIA  KIKAO CHA HARUSI.

MKUU WA POLISI IGP SAIDI MWEMA AMETHIBITISHA TUKIO HILO NA TAYARI MKUU WA UPELELEZI WA MAKOSA YA JINAI WA JESHI HILO (DCI) ROBERT MANUMBA AKIWA NA KIKOSI CHA MAKACHERO WAMEELEKEA MWANZA KUONGEZA NGUVU KATIKA UPELELEZI MKALI AMBAO UMESHAANZA.

HABARI ZAIDI ZINAKUSANYWA NA TUTAKULETEA KWA KINA BAADA YA MUDA SI MREFU.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. poleni sana familia ya kamanda,hawa makamanda wawekewe ulinzi saa zote kazi yao ni risk sana wana maadui wengi!

    ReplyDelete
  2. Kama jukumu lao linazalisha maadui wengi kwa nini wasiwe na Ulinzi wa Vijana wa kazi wanapokuwa ktk misafara yao binafsi?

    Hii itasaidia kama isipofanyika wimbi hili litakuwa kila kukicha!

    ReplyDelete
  3. Poleni wafiwa.Hao makamanda wanatakiwa kuwa wabunifu kwanini neighbour hood watch (sungu sungu)isirudi? Au mpaka mkuu wa nchi aseme?

    ReplyDelete
  4. Hii ni hatari sana. Watu wana "guts" za kumua RPC tena wa jiji kubwa kama la Mwanza? Tunakoelekea sio kuzuri. Polisi waache kuchekeana na wezi/wala-rushwa/majambazi... Msako mkali kwenda mbele 24hrs/day; 365days/year....

    ReplyDelete
  5. Pole sana kwa familia. Sielwei Tanzania inaelekea wapi, yaani kila iitwapo leo ni afadhali ya jana. Mara makanisa yanavunjwa, mara mwandish wa habari ameuawa, mara hiki mara kile, ni nini kinachoendelea? Ni watu wamekata tamaa ya maisha au? Wakati wa baba wa Taifa Mwl Nyerere tunaambiwa maisha yalikuwa magumu zaidi ya na sidhani hali ya matukio haya mabaya ilikuwa kama ilivyo sasa. Nafaikiri kuna tatizo mahali, inabidi tujiangalie upya.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...